Showing 1-20 of 40 items.

WANAULIZANA nini?

Ile khabari kuu,

Ambayo kwayo wanakhitalifiana.

La! Karibu watakuja jua.

Tena la! Karibu watakuja jua.

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

Na milima kama vigingi?

Na tukakuumbeni kwa jozi?

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

Na tukaufanya usiku ni nguo?

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;

Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,

Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.

Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,

Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.